Saturday, 28 January 2017

Vita vyarejea tena Sudan ya Kusini

Mapigano yamerejea nchini Sudan Kusini kati ya serikali na waasi walio watiifu kwa aliyekuwa makamu wa rais nchini humo Riek Machar.
Ripoti kutoka kwa jimbo lenye utajiri wa mafuta la Upper Nile zinasema kumekuwa na mapigano makali ndani na nje ya mji wa Malakal ,ambapo wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wanawahifadhi watu walioachwa bila makao.
Msemaji wa jeshi amesema kuwa idadi ya watu waliojeruhiwa haijulikani kwa kuwa vita hivyo vinaendelea.
Umoja wa Mataifa umezitaka pande hasimu kusitisha uadui na kutekeleza makubaliano ya amani ya mwaka 2015.

Juhudi za kuwanusuru wachimbaji wadogo wa migodi waliofukiwa na Kifusi yaendelea vizuri, Kwa habari kamili Soma hapa


MJMBA JAXWakati imeelezwa kuwa waokoaji katika mgodi wa dhahabu wa RZ Union ulioko Geita , wamebakiza mita tatu kuwafikia waliofukiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Medard Kalemani akizungumza na ndugu wa watu waliofukiwa amesema kwamba wanafanya mpango wa kuwapelekea chakula wachimbaji hao.



Amesema kwamba jana wamefanikiwa kufanya mawasiliano na wachimbaji hao na kwamba wapo kumi na watano na kuwa wanachohitaji kwa sasa ni chakula.


Alisema waokoaji walifanikiwa kuwafikishia kamba na kalamu watu hao ambao waliandika majina na mahitaji yao na kusema kwamba wote wapo salama.


Watu hao akiwemo raia wa China mmoja walifukiwa na kifusi juzi usiku baada ya udongo kukatika na kuziba mlango waliokuwa wakitumia kuingia na kutoka na uokoaji unaendelea kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya uokoaji.

Watu wengi wapo katika eneo hilo wakiwemo ndugu wa waliofukiwa lakini kwa juhudi wanazoziona za uokoaji wametulia na kufuata maelekezo wanayopewa ikiwemo kukaa mita 500 toka eneo la tukio.
Soma hapa ujumbe waliotuma
hata hivyo juhudi za kuwaokoa kutoka chini ya mgodi inaendelea vizuri ambapo matumaini ya kuwapata hai wote inaonekana

Yasome Magazeti Ya Leo Jumapili 29 Jan Hapa

MJMBA JAX


























MJMBA JAX